Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.0 limetokea leo karibu na kisiwa cha Rhodes katika eneo la Mediterania.
Tetemeko hilo lilitokea saa 4:55 usiku, kituo cha uchunguzi cha Kandilli cha Uturuki kimesema.
Mitetemeko iliyosababishwa na tetemeko hilo ilisikika katika majimbo ya Uturuki ya Antalya, Muğla na miji mingine ya pwani ya Aegean na Mediterania.
USGS imeripoti ukubwa wa tetemeko hilo kuwa 5.6.
Hakukuwa na ripoti za kifo au majeraha.



