Kama sehemu ya makubaliano, eneo jipya la Mindanao litaitwa Bangsamoro na Waislamu watakuwa na mamlaka pana.Wakisherehekea makubaliano hayo kwa kupamba mitaa yao kwa bendera za kijani, zinazowakilisha amani, watu wa Mindanao wanachukulia makubaliano hayo kama hatua ya kwanza katika mchakato wa amani.
Waislamu wa Mindanao wanatumai kuwa makubaliano yaliyofikiwa yatawapa haki mpya za kiuchumi, kijamii na kisiasa ifikapo mwaka wa 2016.
Serikali ya Ufilipino na Muungano wa Ukombozi wa Kiislamu wa Moro Jumatatu walitia saini mkataba wa kihistoria wa amani ili kumaliza takriban miongo minne ya mzozo wao uliogharimu makumi ya maelfu ya maisha.
Makubaliano ya awali - yaliyofikiwa baada ya miaka 15 ya mazungumzo yaliyosimamiwa na Malaysia - yanajumuisha ramani ya njia ya suluhu la mwisho ambalo lingeruhusu eneo linalojitawala linalosimamiwa na Waislamu walio wachache kusini mwa nchi hii yenye Wakatoliki wengi.
Makubaliano hayo yalitiwa saini katika hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Rais ya Malacanang ya Manila kwa kushirikisha Rais Benigno Aquino III na kiongozi wa Front ya Ukombozi AL Haj Murad Ebrahim. Wengine waliohudhuria sherehe hizo ni Waziri Mkuu wa Malaysia Najib Razak, katibu mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu Ekmeleddin Ihsanoglu pamoja na wakuu wa balozi za kigeni akiwemo Balozi wa Uturuki nchini Ufilipino Hatice Pinar Isik.
Takriban elfu 120 wameuawa na watu milioni mbili wamelazimika kuondoka makwao katika mzozo huo uliodumu kwa miaka 40.
(Shirika la Habari la Anatolia)



