Data kuhusu kinasa sauti cha ndege ya Urusi aina ya Su-24 iliyodunguliwa na wapiganaji wa F-16 wa Uturuki tarehe 24 Novemba, kwa sasa haiwezi kusomeka kwa mujibu wa jeshi la Urusi, ambalo lilikuwa na matumaini kwamba data hizo zingethibitisha kwamba ndege hiyo haikuingia kwenye anga ya Uturuki. Kazi itaendelea kwenye kinasa sauti, lakini chipsi 13 kati ya 16 zimeharibiwa kabisa.
Uturuki inasisitiza kuwa ndege hiyo iliingia na kupuuza maonyo ya kuondoka kwenye anga yake. Tukio hilo limesababisha mtafaruku mkubwa katika uhusiano kati ya nchi hizo mbili, huku Urusi ikiweka vikwazo na kutaka Uturuki iombe radhi.



