Mlipuko mkubwa uliotokea mjini Ankara umesababisha vifo vya watu 28 na wengine 61 kujeruhiwa, maafisa wa Uturuki wamesema.
Gari lililojaa vilipuzi lililipuliwa huku mabasi ya kijeshi yakipita. Mlipuko huo ulitokea karibu na bunge na makao makuu ya jeshi la Uturuki.
Maafisa wa Uturuki wamekiita "kitendo cha kigaidi."
Baadhi ya wahasiriwa walikuwa raia.



