Lance Armstrong amepokonywa mataji yake saba ya Tour de France na kufungiwa maisha yake yote baada ya Umoja wa Kimataifa wa Uendeshaji Baiskeli kusema leo kuwa umeidhinisha vikwazo vya Shirika la Kupambana na Matumizi ya Dawa za kuongeza nguvu nchini Marekani, Reuters iliripoti.
Uamuzi huo ulitangazwa katika mkutano wa wanahabari wa UCI.
(Shirika la Habari la Anatolia)



