Iran iliibuka kutoka kwa miaka ya kutengwa kiuchumi wakati mataifa yenye nguvu duniani yalipoondoa vikwazo kwa ajili ya Tehran kupunguza matarajio yake ya nyuklia.
Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) mjini Vienna ulithibitisha kuwa masharti yaliyowekwa baada ya mazungumzo makubwa Julai mwaka jana yametimizwa, na kutoa njia kwa Iran kuanza tena mauzo ya mafuta.
Ndani ya dakika chache, Marekani iliondoa rasmi vikwazo vya benki, chuma, usafirishaji na vingine.
Katika hatua ya kushangaza, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilitangaza kuachiliwa kwa wafungwa watano wa Kimarekani akiwemo mwandishi wa habari wa Washington Post, Jason Rezaian, kama sehemu ya kubadilishana wafungwa na Marekani. Kwa upande wake, Rais wa Marekani Barack Obama pia aliwasamehe Wairani watatu walioshtakiwa kwa kukiuka vikwazo dhidi ya Iran.



