Timu ya taifa ya Uturuki ya mpira wa wavu ya wanawake ilifanikiwa kutinga kwenye michuano ya Olimpiki ya London 2012 kwa ushindi mnono wa 25-22, 25-22, 25-20 dhidi ya Poland jana, katika fainali ya michuano ya kufuzu Ulaya.
Maelfu ya mashabiki wakishangilia kwa upande wa Uturuki katika mchezo huo uliochezwa katika ardhi ya nyumbani mjini Ankara, na kuandaa njia ya ushindi wa kihistoria kwa mpira wa wavu wa Uturuki.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Uturuki kuwepo kwenye Michezo ya Olimpiki katika mchezo wa timu tangu 1960 ya Olimpiki ya Roma.
Kabla ya tarehe hiyo, nchi hiyo iliwakilishwa mara sita kwenye soka na mara mbili kwenye mpira wa vikapu. Hakuna timu ya voliboli ya Uturuki iliyowahi kucheza Olimpiki hapo awali.
Uturuki ilikuwa tayari imepata ushiriki wa wanariadha 72 mjini London, ambayo ni rekodi kwa nchi hiyo.



